About Me

My photo
My Name is Neema Ng'asha C.E.O and Founder member of Strong Women Foundation.(SWF).

Wednesday, April 2, 2025

Neema Ng'asha miaka 15 katika muziki wa injili

 Neema Ng'asha,ni Muimbaji wa nyimbo za injili kutoka Tanzania. alianza kuimba tangu akiwa mtoto Sunday school.


Lakini ilipofika mwaka 1998 akiwa kidato cha pili Mungu alimupaka mafuta baada ya kushukiwa na Roho Mtakatifu kwa nguvu sana, tangu hapo akaanza kutunga nyimbo za injili.


Akaanzisha band iliyoitwa Jerusalem band ambayo walikuwa wakiimba na dada yake Martha Ng'asha na vijana wengine pale kanisani.


Baada ya kumaliza chuo pale AVU-University of Dar es salaam ,mwaka 2010 alingia studio na kurekodi album yake ya kwanza iliyoitwa USINIPITE MWOKOZI.


Mpaka sasa amerekodi album 3 na single nyingi ikiwemo SALAMA aliyoichia Mwezi March 2025.


Mwaka 2024 alifanikiwa kupata tuzo ya Muimbaji bora wa kike kutoka kampuni ya Eagle's Entertainment.

Bonyeza link hiyo chini kusikiliza wimbo wa SALAMA 👇👇👇👇https://www.youtube.com/watch?v=BzMUgXdqrCQ

2 comments: